fbpx

Mama mjamzito mwenye dalili za CORONA lazima apimwe kabla ya kuzaa

https://mino.dk/covid19/kiswahili/#mama-mjamzito-mwenye-dalili-za-corona-lazima-apimwe-kabla-ya-kuzaa

Mama mjamzito mwenye dalili za CORONA lazima apimwe kabla ya kuzaa

Mama mjamzito mwenye dalili za CORONA lazima apimwe kabla ya kuzaa

19/03/2020 / /

Tarehe 19.03.2020, wizara ya afya, imetoa mwongozo mpya kuhusu njia ya kuwatunza mama wajawazito ambao wameambukizwa na COVID-19, mama aliye jifungua, waume/wenzi wao na mtoto aliye zaliwa.
Kuanzia sasa wanawake wote wajawazito wanapofika hospitalini, lazima wapimwe ugonjwa wa homa kali ya mapavu ya virusi vya CORONA.
Majibu yakionyesha kwamba mama mjamzito ameambukizwa , wafanyakazi, wauguzi, daktari na mkunga lazima wachukue tahadhari na kuvaa vifaa muhimu kama barakoa (maske), ili kuzuia kuambukizwa. Mama mjamzito lazima pia naye avae barakoa (maske).
Ikiwa kuna hofu ya kwamba, mtoto aliye zaliwa ameambukizwa na virusi vya homa kali ya mapavu ya CORONA, kwa kutumia kanuni ya uangalifu atatunzwa kama mtu yeyote ambae ameambukizwa hadi matokeo ya majibu yatapo pokelewa.
Zaidi ya hayo:
Mume/mwenzio aliyeambukizwa hakubaliwi kuwa wakati wa kuzaa. Hatakubaliwa vile vile, kuwa wakati wa mtoto anazaliwa akishukiwa kuwa ameambukizwa na virusi vya CORONA.
Mume/mwenzio aliyeambukizwa atakiwa kuwa mbali na mtoto aliyezaliwa, masaa 48 kutoka siku ya mwisho ya dalili hizo.
Hospitali nyingi wakati huu zinahimiza kupunguza kiwango cha jamaa hospitalini. Atakubaliwa pekeyake mume/mwenzio wakati wa kujifungua ili kupunguza uwezekano wa uambukizaji.
Licha ya kwamba mama ameambukuzwa na COVID-19, hatatengwa kutoka kwa mtoto mchanga isipokuwa mama yuko katika hali mbaya ambayo anahitaji matibabu.
Ikiwa majibu yaonyesha kwamba mama ameambukizwa na magonjwa lakini haitaji matibabu , inashauriwa arudi nyumbani kutoka hospitalini haraka iwezekanavyo. Mama atapata maelezo jinsi ya kutunza afya ya mtoto nyumbani.

Relaterede nyheder

Ufunguzi wa Denmark awamu ya tatu

08/06/2020
Kuanzia jumatatu tarehe 8 juni 2020, Denmark itafungua tena sehemu zaidi. Hii itajumuisha: Vitengo za michezo za ndani-(michezo za video), […] Læs mere… Læs mere…

Mipaka imefunguliwa kwa kiwango kidogo, lakini unashauriwa kutosafiri nje ya nchi

29/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 29 mai 2020 Serikali imetoa ushauri wa kutosafari […] Læs mere… Læs mere…

Sasa unauwezo mwenyewe wa kupata muda wa kupimwa virusi vya corona- hata ikiwa hauna dalili

19/05/2020
Sio lazima tena kupata rufaa kutoka kwa daktari wako ili uwe na uwezo wa kupata muda wa kupimwa virusi vya […] Læs mere… Læs mere…

Serikali inawasilisha mkakati mpya wa kupima na kufuatilia wale walio ambukizwa

13/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 12 mai 2020 Hivi karibuni Denmark imeongeza sana, […] Læs mere… Læs mere…

Mamlaka ya teknolojia na usalama inatoa onyo dhidi ya barakoa zinazotengenezwa nyumbani

12/05/2020
Watu binafsi wameanza kushona na kutengeneza barakoa wenyewe nyumbani. Walakini barakoa zinazo shonwa hapo nyumbani zinafanya mtu ajihisi yuko salama, […] Læs mere… Læs mere…

Awamu ya 2 kufungua denmark upya inaaza sasa

07/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari tarehe 7 Mei , kutoka kwa Waziri Mkuu Mette Frederiksen Wananchi wote hapa […] Læs mere… Læs mere…

Wizara ya afya imebadilisha ufafanuzi wa ’vikundi vya watu walio hatarini’

06/05/2020
Baada ya kufanya kazi na ufafanuzi mpana sana wa vikundi vya watu walio hatarini kwa maambukizi ya COVID-19, Wizara ya […] Læs mere… Læs mere…

Kwa sasa, vikundi vilivyochaguliwa vya watu walio katika hatari kubwa ya maambukizi watapata chanjo ya bure kwa ugonjwa wa nimonia

04/05/2020
Watu walio katika hatari kubwa ya kuwa wagonjwa zaidi kwa maambukizo ya COVID-19, kwa sasa wanaweza kuwasiliana na daktari wao […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri wa afya na mamlaka ya afya, tarehe 20 aprili 2020

23/04/2020
Tuko katika hatua ya kwanza ya kufunga tena jamii yetu na shughuli za kila siku. Hii ni kwa sababu tumepata […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 14 aprili 2020

14/04/2020
Kwa sasa tunaweza kufurahia vile maendeleo ya virusi vya corona inavyo onyesha hapa nchini Denmark. Nambari zinaendelea kuwa zaidi na […] Læs mere… Læs mere…

Vær med til at sikre
et ligeværdigt Danmark
– for alle!

Sammen styrker vi minoritetsetniske danskeres
muligheder, stemmer og samfundsdeltagelse



Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.

Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.