fbpx

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 6 aprili 2020, saa mbili usiku (Kl.20.00).

https://mino.dk/covid19/kiswahili/#muhtasari-wa-mkutano-kwa-waandishi-wa-habari-kutoka-kwa-waziri-mkuu-tarehe-6-aprili-2020-saa-mbili-usiku-kl-20-00

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 6 aprili 2020, saa mbili usiku (Kl.20.00).

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 6 aprili 2020, saa mbili usiku (Kl.20.00).

06/04/2020 / /

Maendeleo ilivyo sasa ni thabiti na nambari zinaendelea sawa: watu 503 wamelazwa hospitalini, watu 139 wamelazwa katika kitengo cha utunzaji maalum, na watu 187 kwa bahati mbaya wameaga dunia.
Waziri mkuu anabainisha kuwa, virusi huhisiwa kwanza baada ya wiki tatu au nne baada ya maambukizo,na kwa hivyo kuna wasiswasi, kuwa watu wengine wataanza kutozingatia maagizo kwa mfano kwa kusherekea pasaka pamoja.
Kwa msingi huo, waziri mkuu amewasilisha mpango ya kwanza, awamu ya kuanza kufungua tena Denmark. Vidokezo vyote vya mipango ni kwa masharti kuwa kila mtu anachukua jukumu na kuendelea kufuata maagizo ya mamlaka: kuosha mikono, na kukaa mbali mbali na kutokutana na watu wengi.

  1. Awamu ya kwanza ya ufunguzi inajumuisha:
  • Huduma ya afya itafunguliwa tena kwa shughuli nyingine mbali na corona.
  • Vituo vya kulea watoto (vuggestuer,børnehaver,SFO) na shule, madarasa ya 0-5 yatafunguliwa tena.
    o Katika taasisi hizi hatua kadhaa mpya za utunzaji zitatumiwa, njia na mwelekeo mpya wa kuzingatia usafi. Ufunguzi utafanyika kwanza, mipangilio haya yakiwa tayari.
  • Wafanyikazi wa kibinafsi kwa kuzingatia maagizo ya afya wataanza kazi tena.

Waziri mkuu anasisitiza kwamba, haya yote ni kwa masharti kwamba, maendeleo yata kuwa thabiti- na kwamba sisi sote tunayo jukumu la kuhakikisha kwamba inawezekana, kwa kufuata miongozo.
Kwa kuongezea, hatua zingine lazima ziongezwe muda kwa wiki nne zaidi hadi tarehe 10 mei.2020, haya yanahusu:

  • Kufungwa kwa mipaka.
  • Kupiga marufuku mukusanyiko zaidi ya watu 10.
  • Miongozo mikali.
  • Masomo ya vio vikuu, maktaba, sinema, maduka makubwa(storcenter), mikahawa zitaendelea kufungwa.
  • Biashara ndogo ndogo kama vile watunzaji wa nywele, tatoo na kadhalika, bado zitafungwa.

Waziri mkuu anahimiza watu wote wawe wavumilivi na kuelewa, hakuna kitu kitakuwa sawa kama hapo awali- na maisha ya kila siku hayatarudi kama kawaida kwa miezi kadhaa.
Kwa kuongezea anatangaza maswala kadhaa kuhusu:

  • Wanafunzi wa darasa la 6-10 wataendelea kuhudhuria masomo wakiwa nyumbani, lakini mitihani ya mwisho wa mwaka imehairishwa na badala yake kupewa matokeo ya mwaka (årskarakter).
  • Wanafunzi wanaomaliza masomo ya sekondari (ungdomsuddanelse), watalazimika kufanya mitihani yao kwa njia tofauti.
  • Sherehe kubwa, masoko ya nje na hafla zingine kubwa katika msimu wa kiangazi (summer) haitawezekana kufanyika . Marufuku ya mikutano mikubwa yataendelea hadi mwezi wa agosti.
  • Serikali na vyama vya bunge vitaangalia ikiwa vifurushi vya misaada
    (hjælpepakkerne) vinaweza kuboreshwa.

Kwa kuongezea waziri mkuu anasisitiza wito wake wa kuonyesha ushikamano na wito wa jamii, wakati huu haswa kwa benki na kampuni kubwa za kukodisha, wanahitajika kuonyesha muungano. Wananchi pia wanahimizwa kuinua uchumi na kukuza biashara na kampuni ndogo.
Kuhusiana na mfumo wa afya, waziri mkuu ametangaza watu wengi wamepimwa, ili kueleza ni watu wangapi ambao wamekuwa na corona, vile vile wanafanya bidii ili kuhakikisha kuwa wafanyakazi wa huduma ya afya wanavyo vifaa vyote vinavyo hitajika.
Mwishowe, waziri mkuu anasema jambo muhimu zaidi ni kwamba sote tunachangia: ni jukumu la kila mtu kufuata maagizo. Haya ndio masharti kwa jamii yetu kufunguliwa tena pole pole.

Relaterede nyheder

Ufunguzi wa Denmark awamu ya tatu

08/06/2020
Kuanzia jumatatu tarehe 8 juni 2020, Denmark itafungua tena sehemu zaidi. Hii itajumuisha: Vitengo za michezo za ndani-(michezo za video), […] Læs mere… Læs mere…

Mipaka imefunguliwa kwa kiwango kidogo, lakini unashauriwa kutosafiri nje ya nchi

29/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 29 mai 2020 Serikali imetoa ushauri wa kutosafari […] Læs mere… Læs mere…

Sasa unauwezo mwenyewe wa kupata muda wa kupimwa virusi vya corona- hata ikiwa hauna dalili

19/05/2020
Sio lazima tena kupata rufaa kutoka kwa daktari wako ili uwe na uwezo wa kupata muda wa kupimwa virusi vya […] Læs mere… Læs mere…

Serikali inawasilisha mkakati mpya wa kupima na kufuatilia wale walio ambukizwa

13/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 12 mai 2020 Hivi karibuni Denmark imeongeza sana, […] Læs mere… Læs mere…

Mamlaka ya teknolojia na usalama inatoa onyo dhidi ya barakoa zinazotengenezwa nyumbani

12/05/2020
Watu binafsi wameanza kushona na kutengeneza barakoa wenyewe nyumbani. Walakini barakoa zinazo shonwa hapo nyumbani zinafanya mtu ajihisi yuko salama, […] Læs mere… Læs mere…

Awamu ya 2 kufungua denmark upya inaaza sasa

07/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari tarehe 7 Mei , kutoka kwa Waziri Mkuu Mette Frederiksen Wananchi wote hapa […] Læs mere… Læs mere…

Wizara ya afya imebadilisha ufafanuzi wa ’vikundi vya watu walio hatarini’

06/05/2020
Baada ya kufanya kazi na ufafanuzi mpana sana wa vikundi vya watu walio hatarini kwa maambukizi ya COVID-19, Wizara ya […] Læs mere… Læs mere…

Kwa sasa, vikundi vilivyochaguliwa vya watu walio katika hatari kubwa ya maambukizi watapata chanjo ya bure kwa ugonjwa wa nimonia

04/05/2020
Watu walio katika hatari kubwa ya kuwa wagonjwa zaidi kwa maambukizo ya COVID-19, kwa sasa wanaweza kuwasiliana na daktari wao […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri wa afya na mamlaka ya afya, tarehe 20 aprili 2020

23/04/2020
Tuko katika hatua ya kwanza ya kufunga tena jamii yetu na shughuli za kila siku. Hii ni kwa sababu tumepata […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 14 aprili 2020

14/04/2020
Kwa sasa tunaweza kufurahia vile maendeleo ya virusi vya corona inavyo onyesha hapa nchini Denmark. Nambari zinaendelea kuwa zaidi na […] Læs mere… Læs mere…

Vær med til at sikre
et ligeværdigt Danmark
– for alle!

Sammen styrker vi minoritetsetniske danskeres
muligheder, stemmer og samfundsdeltagelse



Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.

Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.