fbpx

MUKUTANO KWA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 17.03.2020

MUKUTANO KWA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 17.03.2020

17/03/2020 / /

Waliohudhuria:
Waziri mkuu Mette Frederiksen,Waziri wa afya Magnus Heunicke, Mkurugenzi wa huduma ya afya
Søren Brostrøm, na mwakilishaji kutoka wizara ya uhamiaji na Mkurugenzi wa Polisi Torkild
Fogde.


Waziri mkuu alianza kwa kusisitiza umuhimu vile hali ilivyo kwa sasa, na inaendelea kuwa mbaya.


Watu 82 wamelazwa hospitalini, kati yao, watu 18 wamelazwa katika kitengo cha utunzaji maalum, hii ikiwa mara dufu kwa siku moja. Kwa hivyo ni muhimu tukomeshe maenezi ya haya maambukizi. Mipango mpya inawasilishwa kuanzia kesho tarehe 18.03.2020 saa 10.00 –mchana, hadi tarehe 30.03.2020.

Mikusanyiko ya watu kuzidi 10 imepigwa marufuki, ndani na nje, kwa hafla za umma. Unashauriwa usikusanyike zaidi ya watu 10 kwa mipango au faragha ya kibinafsi.

  • Vikwazo zaidi zimewekwa kuhusu maduka: lazima kuwe na nafasi ya kutosha kati ya watu,
    umbali wa kutosha, wateja wawe na uwezo wa kuaosha mikono, ndani na nje ya maduka.
  • Vituo vyote vya michezo na mazoezi ya ndani vitafungwa, kwa mfano vituo vya mazoezi
    ya gym, duka za kutengeneza nywele, tattoo- Kwa ujumla wafanyaji biashara –kwa sababu
    ya asili ya kazi yao wako karibu na wateja. Haya vikwazo haijumuishi wale ambao
    wanapeana matibabu.
  • Vilabu vya usiku, mikahawa ya kuvuta sigara, (vandpibecafeer) na mastarehe zote lazima
    zifungwe.
  • Vituo vya kuota jua bandia (solcenter),mahala pa kuchezea video (video games)- lakini sio
    maduka ya kuuza vyakula kwa vituo vikuu, lazima zifungwe.
  • Mikahawa,hoteli na kadhalika inapaswa kufungwa- lakini chakula ya kununua na kwenda
    nayo itaendelezwa.
  • Wadanish wote wanaorejea nyumbani kutoka nje ya nchi , wajiaondoe katika orodha
    iliyotengwa , ikiwa wamesajiliwa tena na kwenda nyumbani kwa hiari yao na kujitenga
    kwa siku 14.

    Heunicke, Brørstrøm na Føgde walisisitiza uzito wa hali ilivyo kwa sasa. Ni wakati huu inabidi kuchukua hatua kali ikiwa tunataka kuepuka matokeo mabaya. Hakuna mtu yeyote anayeweza
    kuacha kufuata haya mapendekezo ya wizara ya afya, haya maelezo yakiwalenga haswa, vijana.

    Kama suala la kanuni, waziri mkuu alipendekeza kwamba, ikiwa una shauku juu ya kitu fulani kinachohusiana na afya, kama kwa mfano kula chakula cha jioni pamoja na marafiki, ni heri uache kuhudhuria.
    Waziri mkuu aliwashukuru tena kila mtu ambaye yuko katika kitengo ya maandalizi.

    Kwa kuongezea, waziri mkuu alitangaza vifurushe vipya vya misaada (hjælpepakker), kwa wafanyakazi wanaoajiriwa na waliojiajiri na kwa makampuni. Bunge itajadiliana kuanzia mapema kesho kati ya vyama tofauti. Polisi watapatikana zaidi ya kawaida kwa kuwashauiri na kuwaongoza raia. Wizara ya mambo ya nje inakadiria kuwa kuna wadanish wengi ambao wamekwama nchi za nje, na
    anawashauri kwamba watafute mahala pazuri pa kukaa. Danmark itawaleta nyumbani haraka iwezekanavyo.

Relaterede nyheder

Ufunguzi wa Denmark awamu ya tatu

08/06/2020
Kuanzia jumatatu tarehe 8 juni 2020, Denmark itafungua tena sehemu zaidi. Hii itajumuisha: Vitengo za michezo za ndani-(michezo za video), […] Læs mere… Læs mere…

Mipaka imefunguliwa kwa kiwango kidogo, lakini unashauriwa kutosafiri nje ya nchi

29/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 29 mai 2020 Serikali imetoa ushauri wa kutosafari […] Læs mere… Læs mere…

Sasa unauwezo mwenyewe wa kupata muda wa kupimwa virusi vya corona- hata ikiwa hauna dalili

19/05/2020
Sio lazima tena kupata rufaa kutoka kwa daktari wako ili uwe na uwezo wa kupata muda wa kupimwa virusi vya […] Læs mere… Læs mere…

Serikali inawasilisha mkakati mpya wa kupima na kufuatilia wale walio ambukizwa

13/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri Mkuu, tarehe 12 mai 2020 Hivi karibuni Denmark imeongeza sana, […] Læs mere… Læs mere…

Mamlaka ya teknolojia na usalama inatoa onyo dhidi ya barakoa zinazotengenezwa nyumbani

12/05/2020
Watu binafsi wameanza kushona na kutengeneza barakoa wenyewe nyumbani. Walakini barakoa zinazo shonwa hapo nyumbani zinafanya mtu ajihisi yuko salama, […] Læs mere… Læs mere…

Awamu ya 2 kufungua denmark upya inaaza sasa

07/05/2020
Muhutasari wa mkutano kwa waandishi wa habari tarehe 7 Mei , kutoka kwa Waziri Mkuu Mette Frederiksen Wananchi wote hapa […] Læs mere… Læs mere…

Wizara ya afya imebadilisha ufafanuzi wa ’vikundi vya watu walio hatarini’

06/05/2020
Baada ya kufanya kazi na ufafanuzi mpana sana wa vikundi vya watu walio hatarini kwa maambukizi ya COVID-19, Wizara ya […] Læs mere… Læs mere…

Kwa sasa, vikundi vilivyochaguliwa vya watu walio katika hatari kubwa ya maambukizi watapata chanjo ya bure kwa ugonjwa wa nimonia

04/05/2020
Watu walio katika hatari kubwa ya kuwa wagonjwa zaidi kwa maambukizo ya COVID-19, kwa sasa wanaweza kuwasiliana na daktari wao […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa waziri wa afya na mamlaka ya afya, tarehe 20 aprili 2020

23/04/2020
Tuko katika hatua ya kwanza ya kufunga tena jamii yetu na shughuli za kila siku. Hii ni kwa sababu tumepata […] Læs mere… Læs mere…

Muhtasari wa mkutano kwa waandishi wa habari kutoka kwa Waziri Mkuu tarehe 14 aprili 2020

14/04/2020
Kwa sasa tunaweza kufurahia vile maendeleo ya virusi vya corona inavyo onyesha hapa nchini Denmark. Nambari zinaendelea kuwa zaidi na […] Læs mere… Læs mere…

Vær med til at sikre
et ligeværdigt Danmark
– for alle!

Sammen styrker vi minoritetsetniske danskeres
muligheder, stemmer og samfundsdeltagelse



Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.

Hvert eneste medlemskab og donation styrker Mino Danmarks legitimitet og eksistensberettigelse.

Det gør en forskel og styrker foreningens muligheder for at lykkes med at skabe et lige samfund, uanset etnisk baggrund.